Advertisements

Thursday, March 5, 2015

Kizaazaa cha albino walipotifuana huko Ikulu

Baadhi ya watu wakiamulia ugomvi uliotokea kati ya wanachama na viongozi wao.

WATU wenye ulemavu wa ngozi (albino), leo walizusha vurugu katika viwanja vya Ikulu wakipinga baadhi ya wao kuonana na Rais Jakaya Kikwete.

Kundi la albino waliokuwa wamebaki nje walianza kupaza sauti na kudai waliopewa nafasi ya kuingia kuonana na Mhe. Rais si viongozi wao, jambo ambalo liliwalazimu maofisa usalama kuingilia kati.

Katika mkutano huo, Rais Kikwete alikutana na wawakilishi 15 huku wengine zaidi ya 30 wakiwa nje na kuanza kupaza sauti zao na kusema kuwa walioingia ndani sio viongozi wao kwani muda wao ulishakwisha hivyo ni bora wakatoka kabla hawajaanzisha vurugu kubwa katika eneo hilo.
Ofisa wa Ikulu akiwazuia albino baada ya kutokea mtafaruku na viongozo wao kabla ya kuingia Ikulu ambapo Rais Kikwete alikuwa na mazungumzo na baadhi ya viongozi wao.
Watu wenye ulemavu wa ngozi wakijaribu kutupiana makonde nje ya Ikulu muda mfupi kabla ya kwenda kuonana na rais jakaya kikwete ambaye alikuwa na mazungumzo nao.


Picha na taarifa: Habari Mseto blog

1 comment:

Anonymous said...

hatari sana pesa inaweza kuuwa bwana kuna mmoja wao alichimba mkwara pale kutaka kumtoa roho mwezake,"tutakuuuwa sisi wewe"
na jamaa alinifurahishia sana aligeuka kuwa van damme lazima atakuwa kapitia jkt alirusha teke huyo haaaaaaaaaaa.

but all in all ikulu ni sehemu muhimu na inastahili iheshimiwe. but kila mtu anapiga deal kule hakuna tena heshima kule.

walichimbiana wenyewe mikwara baadaya wakaenda kunywa juisi kwa mheshimiwa. haaaaaaaaaaaaaaaaa.

shikamoo pesaaaaaaaaaaaa.

albino wa dar hawwa sio wanauliwa ni wala wa lake zone ndo wako kwenye hatari hawa huoni wanapigania ruzuku bwana na ukuu na kutaka kwenda kuchukua pesa na kunywa juisi.

yani nilivyokuwa nawaona kwenye kioo changu niliburudika sana.

pesa shikamooo,shikamooooo.pesa inakufanya umtoa roho hata mama yako mzazi. ni shidaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.