Advertisements

Wednesday, April 9, 2014

INATIA HURUMA JINSI SIMBA ALIVYOMUUA NYANI HUYU MWENYE MTOTO ,UNAJUA NINI ALIKIFANYA KWA MTOTO WA NYANI?

Mpiga picha Evan Schiller na Lisa Holzwarth wametumia muda wao wa kutosha tu kuchukua picha za tukio la kusisimua na kusikitisha huko Botswana baada ya kushuhudia nyani mwenye mtoto akikumbana na hasira za simba jike mwenye njaa ambaye alimfukuza na hatimaye kumkamata na kumuua.
Nyani huyo aliuawa huku mtoto wake mchanga akiwa amemkumbatia pasipokujua kuwa mama yake tayari alikuwa ameshakufa. baada ya simba kuua nyani huyo sasa kibao alikigeuzia kwa mtoto ambapo aliaanza kumtisha pamoja na mtoto huyo wa nyani kutaka kukimbia simba alimkamata tena. chanzo tabianchi

Baadae mtoto wa nyani alianza kucheza na simba na kumfanya kama mamayake. Tazama picha uone tukio kamili hatua kwa hatua.
Simba akiwa amembeba nyani baada ya kumuua, huku mtoto wa nyani akiwa amemkumbatia mama yake bado
Muda mfupi, mtoto wa nyani alitaka kutoroka lakini alishindwa kupanda mti, sasa simba akamfuata kuona nini kinaendelea.
Lakini cha ajabu badala ya simba kumuua mtoto huyo wa nyani alianza kucheza naye na kukafanya kanyani kasahau machungu.
hapa sijui nyani mtoto anawaza nini, weee usicheze na simba jamani.
Wacha weee, sasa hapa simba sijui ndo kamsamehe kweli huyu nyani au ndo amemuweka kiporo njaa ikiuma amtafune, lakini mtoto wa nyani anaonekana kuenjoy tu.
Nyani mtoto kashapagawa na joto la simba, anaanza kutafuta kunyonya kifuani kwa simba, ana hatari huyu mtoto.
Raha iliyochanganyikana na hofu, hatari tupu
Wasije simba wengine! simba jike akaanza kuwatimua sasa sijui alikuwa anakalinda katoto ka nyani kasiliwe au aliona wenzake watammalizie msosi wake wa baadae.
Haa! kumbe baba nyani alikuwa kando akifuatilia issue yote na wakati simba wanazinguana akapata upenyo wa kumuokoa mwanaye na kupanda nae kwenye mti, uuuh kweli kama siku yako haijafika unaweza hata kumkamua maziwa simba na akabaki kukuchekea tu
Stori hii ni ya kufurahisha, huzunisha na kushangaza na inaonyesha ni kwa kiasi gani kila jambo limepangwa kwa maksudi yake na kwamba hata tukiwa katika magumu ya hali gani ukombozi unaweza kupatikana kikubwa tu ni kujiamini kama mtoto wa nyani alivyofanya.
chanzo:Tabianchi blog

4 comments:

Anonymous said...

binadamu tumepewa akili na mungu lakini hatupo namna hivi kabisa tutauwa mama nyani na nyani mwenyewe eti kuvuruga ushahidi au kwa unyama na ukatili wetu tizama simba kamuachia mtoto wa nyani tunajifunza nini kwa wanyama sisi binadamu?

Anonymous said...

Du Mpwa umenenepa.

Anonymous said...

Wow!

Anonymous said...

hapo nimejifunza huruma, Wanyama wana huruma kuliko mwanadamu,