Advertisements

Monday, May 13, 2013

SAKATA LA WASICHANA 11 KUSHOOT VIDEO YA NGONO NA MBWA , VIONGOZI WA DINI WAJA JUU

Habari iliyosambaa hivi sasa kupitia mitandao ya jamii nchini Kenya na kuwashangaza wakenya wengi ni kuhusu mwanaume mmoja raia wa kigeni na wasichana 11 waliokamatwa Mombasa kwa tuhuma za kushoot video ya ngono na mbwa.
Kwa mujibu wa Baraza la Maimamu na Wahubiri wa Kenya (CIPK) tukio hilo ni la aibu kwa jamii na inahitaji kukemewa. viongozi hao wametoa wito kwa polisi kufanya uchunguzi kamili na kuhakikisha kuwa pande zote zinazohusika zinafikishwa mbele ya sheria bila woga au upendeleo. Viongozi hao wamebainisha kuwa baadhi ya matukio yanachangiwa na ukosefu wa msimamo kutoka kwa viongozi wa serikali na viongozi wa juu, juu ya masuala hayo.
'Hii sasa imefikia hatua ya kusumbua sana, kama binti zetu wanaweza kwenda nje na kulala na mbwa, na ni polisi pekee ndio wanaweza kusimamisha uovu huu,w kwa sababu hata baadhi ya viongozi wetu wa sasa na wa zamani katika serikali kamwe ameshindwa kujitoa na kuonyesha msimamo wao juu ya masuala hayo 'alisema Sheikh Khalifa Mohammed CIPK.

Sheikh Khalifa amebaini kwamba kuna club nyingi za wacheza uchi {stripper} na madanguro hasa Mombasa na Kilifi ambapo wasichana wenye umri mdogo kuwaburudisha wateja wao huku wakiwa uchi na kuwataka viongozi wa serikali na serikali kwa jumla kuzifunga sehemu hizo.

haya ndio majina ya watuhumiwa wa kosa hilo. Janeth Amollo, Christopher Clement Weissenrieder, Mercy Waithera Karanja, Beatrice Mueni Mwosa, Mary Nyambura Kimani, Magdaline Wairimu Chege, Celestine Nekesa Sitati, Dorcus Melisah Indakwa, Lydia Nyaboke Momanyi, Beatrice Mueni Mwosa, Phidelia Mawia Sollomon, Anne Wanjiku Gichuki na Cecilia Nzambi Katuku.

No comments: